Home → ushauri
→ FAHAMU SIRI NZITO KUHUSU FRENCH KISS (DENDA) WAKUBWA TU PLZ
Kama unadhani busu linalohusisha ndimi na mate ni kitu kidogo na cha kawaida basi fikiria mara mbili, yamkini unatenda tendo hili lakini hujui undani wake. Mtaalam mmoja alisema “In the mating game, a kiss is more than a kiss, it is a taste test”.
Mate ya binadamu yanahusisha chembechembe “molecules” kutoka maeneo mbalimbali ya mwili wako, mara ndimi zenu zinapokutana “molecules” hizi hutuma ujumbe katika ubongo wa mwanaume na mwanamke.
Watafiti wamegundua kwamba kuna wingi wa “bioactive testosterone” katika mate ya mwanaume kuliko kwa mwanamke, hali hii huyapa mate ya mwanaume uwezo mkubwa wa kuamsha ndani ya ubongo wa mwanamke hamu na hisia kubwa za kufanya tendo la ndoa.
Hii ndiyo sababu inayofanya wanawake wengi kushindwa kujizuia kufanya tendo la ndoa mara tu wanaporuhusu mwanaume kugusanisha ndimi “tongue/French kiss”.
FAHAMU SIRI NZITO KUHUSU FRENCH KISS (DENDA) WAKUBWA TU PLZ Kama unadhani busu linalohusisha ndimi na mate ni kitu kidogo na cha kawaida basi fikiria mara mbili, yamkini unatenda tendo hili lakini hujui undani wake. Mtaalam mmoja alisema “In the mating game, a kiss is more than a kiss, it is a taste test”. Mate ya binadamu yanahusisha chembechembe “molecules” kutoka maeneo mbalimbali ya mwili wako, mara ndimi zenu zinapokutana “molecules” hizi hutuma ujumbe katika ubongo wa mwanaume na mwanamke. Watafiti wamegundua kwamba kuna wingi wa “bioactive testosterone” katika mate ya mwanaume kuliko kwa mwanamke, hali hii huyapa mate ya mwanaume uwezo mkubwa wa kuamsha ndani ya ubongo wa mwanamke hamu na hisia kubwa za kufanya tendo la ndoa. Hii ndiyo sababu inayofanya wanawake wengi kushindwa kujizuia kufanya tendo la ndoa mara tu wanaporuhusu mwanaume kugusanisha ndimi “tongue/French kiss”.
Artikel Terkait
VITU VIZURI 60 VYA KUMWAMBIA MSICHANA UMPENDAE:  Ninamaanisha kuwa maneno matamu.Wakati kijana uko kwenye process ya kutafuta na kujaribu kuuteka moyo wa msichana, unatakiwa kujifunza kutumia maneno matamu.Na lazima ujue kuwa sio kila neno unalotumia litagusa moyo wa mwanamke unayemtaka,Lakini maneno matamu yanafanya kazi ya kushangaza . Wakati vijana wengine wanalalamika kuwa ni vigumu kuuteka moyo wa msichana, jibu ni rahisi kwa sababu hawatumii maneno sahihi. watu wengi pia huwa hawana maneno ya kusema na wengine hawajui kabisaaa hata jinsi ya kuanza. sasa hebu tujifunze haya maneno ya kumwambia msichana unaempenda na unahitaji awe wako milele. 1.Macho yako ni mazuri , yananifanya nipotelee kwako kila nikiyatizama. 2,Unanifanya niwe mwanaume bora , kwa hio nastahili mapenzi yako. 3.Tumbo langu hutetemeka unapoleta mikono yako usoni pangu. 4.Wewe ni mzuri na ni mrembo naogopa hata kukugusa naona kama nitakuchafua. 5.Unapotabasamu huzuni kwangu hupotea , ghafla nakuwa mtu wa furaha. 6.Ungeweza kupata mwanaume yeyote duniani , lakini umenichagua mimi. 7.Hapana.wewe sio mnene uko poa na ndivyo nipendavyo. 8.Ninapokushika nashisi kulegea kwenye magoti. 9.Wewe ni rafiki yangu, najifunza vitu vingi kwako,ndiye mtu ambae nimekuchagua, ndio mpenzi wa maisha yangu. ni wangu pekee, wewe ndio kila kitu kwangu. 10.Siamini , maana jinsi ulivyo amazing, lakini upo na mimi. 11.kila nikiangalia muda naona kama hautoshi kukupenda , natamani niwe na wewe milele. yaani wasife. 12.Umenifanya niamini kuwa zipo nafsi zinazoungana, zinazokutana pamoja. 13.Usiku nikiwa naangalia nyota na kuzilinganisha kila moja ili kuelewa ni kwa nini nakupenda,nilifanya vizuri hatimae nikazikimbia. 14.Kukutana nawe ni kitu ambacho hakijawahi kutokea. 15.Unapoonyesha kunipenda, huwa nazidiwa na hisia , hapo hupotea kabisaaa. 16.Kabla ya kulala ni lazima kwanza nikupigie simu ndio nitapata usingizi. 17.Naweza kuwa nawe maisha yote, lakini bado nahisi kama haitatosha kukupenda. 18.Napata furaha nikiwa na wewe. 19. Napenda kutumia muda na wewe. 20.Napenda ngozi yako laini, ninapoigusa. 21.Natamani maishsa yangu yote nikuone ukiwa na furaha. 22.Usibadilike nakupenda jinsi ulivyo. 23.Nikiwa na wewe nafurahi kama mtoto. 24.Napenda nywele zako. 25.Napenda nikukumbatie ninapokuaga. 26.Natamani kukubusu kila sehemu ya mwili wako. 27.Naanza siku na wewe ndani ya mawazo yangu, na ninamaliza siku na wewe kwenye ndoto zangu. 28. ukiwa na mimi huwa natamani kusimamisha muda, maana muda unakwenda haraka. 29.Nikisikia sauti yako asubuhi , siku nzima ni mtu wa furaha. 30.Tabasamu lako zuri linanifanya niyeyuke. 31.Unaponiaga napata shida kukuruhusu uende. 32. Umenielewa vizuri, ni kama unasoma mawazo yangu. 33.Mungu alikupendelea kukuumba, akili na kila ulichonacho. 34.Najivunia kuwa na wewe na ninafurahia. 35.Napenda unavyosema unanipenda. 36.Mapenzi yetu ni kama mawimbi ya bahari, wakati mwingi hutulia, na wakati mwingine huvuma,lakini yanarudi palepale. 37.mapenzi yetu yawe kama ua rose ambalo halina miiba. 38.Najua kwa nini watu wanatutazama , ni kwa sababu wewe ni mzuri kuliko mwezi. 39.Muda utakuwa hauna thamani endapo sitatumia na wewe. 40.kama siku yangu ingeanza na busu lako, nisingehitaji kahawa. 41.Kama ningeambiwa nielezee rangi, basi ningeenda kwenye rangi za rainbow, kwa sababu wewe ni mzuri.ni wa muujiza. 42.Mimi bila wewe ni mbaya, lakini ni mzuri nikiwa na wewe. 43.Tukishikana mikono na mioyo yetu inashikana,na nafsi zetu zinapatana . 44.Siku ya kwanza tulipokutana, nilijua ipo siku tutakutana tena, na nafurahi imetokea. 45.Nafurahi tumekua pamoja, sina cha kukosa hata kidogo. 46.Moyo wangu unapumua kama ndege, kila unapotabasamu. 47.Kila ninapokuwa nimeshuka moyo, nikikusikia wewe moyo wangu unapata nguvu. 48.Shika mikono yangu nami nitashika moyo wako, tunza kwa maisha yote. 49.Maisha yote , milele yote,isio na mwisho, toka nimekutana na wewe maneno yote yana maana. 50.Siku naona kama mwaka, na siku inapita kama sekunde. 51.Natamani ningekuwa kama pweza mwenye mikono mingi ili nikukumbatie na mikono myote. 52.Siamini katika nafsi mpya, lakini baada ya kukutana na wewe nimeamini, natamani kama ningeweza kurudi nyuma na kutengeneza kitu. 53.Sitaweza kukutoa kwenye mawazo yangu , kwa maana nakuhitaji uwepo. 54.Kuna wakati nahisi upweke, kwa wakati huo, basi huamua kukupigia simu na kusikia sauti yako. 55.Ninapokutizama namuona mungu jinsi alivyokuumba na kukubariki. 56.Unanifanya niwe wa muhimu . 57.Ni siri ambayo inanifanya nikutazame zaidi kwa kila siku. 58.Kuongea na wewe kila siku unanifanya nikufahamu zaidi na zaidi. 59.Moyo wangu nakupa,nipe moyo wako ili tuifungie kwa pamoja, na tutupe ufunguo mbali. 60.Nakuhitaji muda wote, siku , mwaka na hata milele. ... Read More
KWA WANAWAKE TU! NJIA 14 ZA KUJIWEKA ILI WANAUME WATAMANI KUKUTONGOZA  Je umekuwa ukijiuliza kwa nini haukuwi approached na wanawaume kama unavyotaka? Mtandao wa Sayari ya Mapenzi umeamua kukuandalia mbinu na maujanja ya kutumia ili uonekane mwanamke ambaye anaweza kufukuziwa na mwanaume kwa urahisi. Owk.... Kando na itikadi ambazo umekuwa ukifikiria, kuapproachiwa ama kufukuziwa na mwanaume si gemu ya bahati nasimu ambayo mtu anaingojea ijitokezee. Na pia kando na itikadi nyingi za wanawake wanazozifikia, si lazima ufanye kitendo kikubwa ama cha inadi ili mwanaume aweze kukutongoza. Ukweli ni kuwa, kama unaielewa akili ya mwanaume na jinsi inavyofanya kazi kabla ya kuapproach mwanamke, unaweza kumfanya mwanaume yeyote kutaka kuongea na wewe dakika tano atakapokuja katika himaya yako. So mbinu zenyewe ndizo zipi? Zama nami... Njia za kujiweka ili mwanaume apate nafasi rahisi ya kukutongoza Kwanza jiweke nadhifu Hii ni muhimu katika yote kama wataka mwanaume akutambue. Mwanaume kitu cha kwanza anachokiangalia huwa ni mwonekano wa mwanamke. Mwanaume anapoingia katika chumba, inamchukua sekunde ndogo zana kuamua iwapo anataka kuapproach mwanamke mfani au la. Kama umevalia vizuri na unapendeza, itarahisisha kazi yako sana. Pili usionekane kama una shughli Usijishughlishe sana na simu yako, ama kitabu chako, ama kitu kingine. Unaweza kuwa umeboeka na unajaribu kujiweka buzy, lakini fursa iweza kuwa hivi, kufanya hivyo kunaweza kumfanya mwanaume anayetaka kukuapproach kuona ya kuwa uko buzy sana kiasi cha kuwa atashindwa kukufuata kwanu unaweza usiwe interested na maongezi yake. Tatu ni kuwa mko ligi moja? Hii inakinzana na hatua ya kwanza, lakini inaweza kuwa na tatizo iwapo unaoneka kama uko ligi tofauti na mwanaume. Kama utaoneka amakujiweka mtu wa hadhi ya juu wanawake watapenda kukuangalia lakini hawatakuaproach. Hii ni kwa sababu wanaume wengi hawapendi kudhalilishwa wakati wanapoamua kukuapproach....kiufupi ni kuwa ukiwa unavutia kupindukia wanaume watakuogopa. Lakini tena, kuna wale wanaume ambao wanajiamini kupindukia ambao wanajua thamani ya kukuapproach, nao ni wanaume alfa, wanaume diriki, na pia wale wanaume mapleya. Kama wataka kuteka atenshen ya mwanaume mzuri wa kawaida lakini anayeogopa kukuapproach, jaribu kutumia mbinu ya kuwa jamili na watu wanaokuzunguka. Huwa inasaidia. Ujanja wa kumfanya mwanaume aweze kukuakuaproach 1. Jinsi utakavyovalia Usivalie kana kwamba huna kitu cha kuficha. Utapata atenshen ya kila mtu lakini wanaume ambao wataamua kukuapproach ni wale ambao wanataka kulala nawe kwa usiku mmoja pekee. Enyewe kuvalia kwa kutamanisha kunasaidia kuteka atenshen ya mwanaume, lakini usivuke mipaka ya kawaida. Kumbuka kuwa si lazima uonyeshe viungo vyako vyote vya mwili ili uweze kuteka macho ya mwanaume. Kama unavutia inatosha kumfanya mwanaume akugundue. 2. Unavyomuangalia Mchungulie mara moja na nyingine, halafu mwangalie mara kwa mara. Hakikisha ya kuwa haujisahau ukamwangalia sana kupindukia ama atakuona kama wewe ni rahisi wa kuapproach na anaweza kukupuuza. 3. Mitindo ya kumwangalia Kuna mitindo miwili mikuu ya kumwangalia mwanaume ili kumuonyesha ya kuwa umevutiwa naye. Unaweza kutumia mbinu zote mbili kulingana na vile unataka. i) Kumwangalia polepole - wakati ambapo unaangalia pande zote, angalia upande wake na uyaangalie macho yake kwa sekunde kadhaa huku ukiweka tabasamu. Halafu pole pole zungusha kichwa chako uangalie kwingine. Mbinu hii ni ya kijasiri ya kumwonyesha mwanaume umevutiwa kwake. ii) Kumwangalia kwa uharaka - hii ni mbinu ya kumwangalia kwa uharaka. Anza kumuangalia, ukiona kama anataka kukuangalia, ghafla angalia kando halafu utoe tabasamu ukiangalia chini. Mbinu hii inampa confidence na kukuona wewe ukipendeza. 4.Mfanyie kazi iwe rahisi Inakuwa vigumu kwa mwanaume kumuapproach mwanamke sehemu ambapo yuko kundini na marafiki zake. Kama mawazo yako ni kufuatwa na mwanaume, hakikisha ya kuwa wakati mwingine unajipa time ukiwa pekeako ama zaidi uwe na rafiki yako wa kike mmoja. 5. Sehemu zifaazo Si kila sehemu ni nzuri kufanya maongezi na mtu. Kama unataka mwanaume akuapproach, chagua sehemu ambayo si kila mtu ataanza kujeuza kichwa chake kutaka kujua ni nini kinachoendelea kati yenu. Sehemu za mkawahawa, supermarket, ama bookshop ni sehemu nzuri zaidi za kukutana na mwanaume kupiga stori. 6. Mpatie nafasi aongee na wewe Hata kama uko katika group na marafiki zako halafu mwanaume akakugundua, mwonyeshe interest kwa kumuangalia kwa madakika. Ukiona kama yuko tayari kuongea na wewe, unaweza kujitenga na marafiki zako kwa muda. Aidha unaweza kuanza kuzunguka hio sehemu kiasi ama unaweza kujipeleka mahali ambapo itakuwa rahisi kwa mwanaume huyu kuzungumza na wewe. 7. Tabasamu Onekana jamili, na nafasi ya wewe kufuatwa na wanaume itaongezeka mara dufu. Kupendwa kwa mwonekano wa kwanza ni kama baraka kwa mwanamke yeyote yule ambaye anataka macho ya mwanaume yamwone. 8. Usiboe Kuwa mwanamke mwenye furaha na mwenye hisia chanya mahali popote pale utakapokua. Mwanamke mwenye shangwe huvutia mwanaume yeyote yule. Kama utaonyesha chembechembe za kuboeka, mwanaume anayetaka kukuapproach anaweza kuwa na maswali mengi ya kujiuliza kwani ataona ya kuwa maisha yako huboesha na yasiyo na mwanga. 9. Usiwe mjeuri Kama wewe ni mjeuri kwa yeyote, aidha weita ama mmoja wa rafiki yako, inaweza kutokea kuwa mwanaume ambaye anapania kukuapproach kusimamisha ari yake. Hakuna mtu anapenda mtu mjeuri, na hakuna mwanaume angependa kuapproach mwanamke ambaye anaweza kumpuuzia ama kumkataa. 10. Usitangamane na wanaume Hii ni muhimu kwa mwanamke yeyote aelewe. Usiwahi kamwe kutangamana na marafiki zako wa kiume kama unataka kukuwa approached na mwanaume. Haitafanya kazi kamwe. 11. Mwoneshe kuwa uko intrested Mwonyeshe kuwa uko interested kwake kwa kutaka kumjulia hali zaidi. Hata kama uko na marafiki zako mnaongea halafu amekaa karibu na wewe, mwangalie iwapo anakuangalia hata kama unawajibu rafiki zako. 12. Onyesha uanawake wako Mwangalie mara kwa mara, halafu ukishika macho yake, peta nywele zako nyuma ya sikio lako. Inaweza kuonekana kama jambo dogo kwako, lakini kwa mwanaume ni kama kugonga ndipo. 13. Mtege Pita mbele yake halafu mwangalie machoni mwake wakati unapompita. Mtese kihisia, ataipenda kuona atenshen yake. 14. Usilazimishe Utakuwa unajiaibisha iwapo unalazimisha mambo. Wanaume si mabubwi, hivyo ukiwaangalia mara moja na nyingine ama kuwatabamia, wanajua kuwa uko tayari kuapprochiwa. Ok hizi ni mbinu ambazo unafaa kuzitumia kama unataka mwanaume yeyote yule akunotice ama akufukuzie. ... Read More
NJIA RAHISI 13 ZA KUWA NA FURAHA KILA SIKU  Mabadiliko yalio mepesi kwenye tabia zako za kila siku yatakuweka kwenye mstari wa furaha unayoitaka Umejikuta uko kwenye siku tofauti, story hizo hizo, imekuwa ni kawaida yako? Basi muda huu , sio kesho , sio wiki ijayo, ni wakati wa kubadilisha historia yako. ni za haraka, rahisi na hazina gharama unapofanya hivyo na matokeo yatakupa furaha unayoitaka. 1.Pata masaa 7 mpaka 8 ya kulala usiku. Kulala usingizi wa kutosha unapata furaha, utaweza kuwa na nguvu ya kufanya kazi zako , na utakuwa na mahusiano mazuri. weka simu yako mbali unapoenda kulala, usitumie chakula kingi wakati wa jioni. 2.Amka mapema , dakika 30 kabla . Kama wewe ni mfanya kazi wa kuajiriwa na una tabia ya kuchelewa kazini, jaribu kuamka mapema dakika 15 au 30 kila siku kwa ajili ya kujiandaa vizuri na kukumbuka vitu vyote vya kufanya, kuchukua siku hio. utaona tofauti ya tabia yako. 3.Meditate. Hii ni kubwa. meditate kwa muda wa dakika 10 au 20, utapata faida nyingi zaidi ya furaha, pamoja na kuwa muwazi, kuwa na malengo ya siku nzima. Anza siku yako na meditation. utajiepusha na tress na wasiwasi na hutachanganyikiwa na kazi zako. 4.Jipe nafasi wengi wetu huwa tunajaza vitu nyumbani, ofisini hata vile ambavyo havina kazi, hatuvitumii. inaharibu mfumo mzima wa akili yako, hisia zako, na mwili wako. Ondoa vitu ambavyo huvitumii, tupa nje au gawia watu ambao wanahitaji kuwa navyo, hali yako ya furaha itaboreka. Na hutalemewa na kazi nyingi. 5.Jifunze kitu kipya Jitahidi kujifunza kitu kipya kila siku, kwa sababu hio ndio changamoto itakayokupa furaha, kujifunza kitu kipya inaboresha afya yako ya mwili na akili, kujifunza utajenga ujasiri pia na utakuwa sharp. 6.Tembea mara kwa mara Kutembea kwa dakika 30 kwa siku moyo wako utakuwa unafanya kazi vizuri, utapunguza hasira, hutakuwa na chuki. Kama unaona ni ngumu kwako kutembea , hasa kama una gari , jifunze kupaki gari yako mahali mbali na ofisi , tembea . anza kutumia maji ya kutosha. utapata faida nyingi . 7.Usijihusishe na mambo ya mitandao. Ni rahisi kuingia instagram, facebook na zingine, lakini wachunguzi wanasema kwamba ukizidisha kujihusisha na mitandao unaweza kuharibu afya yako ya akili. badala ya kutumia nusu saa kwenye mitandao, unaweza kufanya kitu kingine unachokipenda, au kusoma kitabu, kujifunza mafunzo mbalimbali kwa ajili ya kujiboresha mwenyewe kuwa mwenye afya. 8.Kuwa mwema. Ukarimu unakuongoza kwenye furaha yako mwenyewe na utakuwa mwenye afya bora. vitu ambavyo vinavyo chochea furaha ni kutoa , na kuwa mkweli , utapata faida , na utajisikia vizuri kuwa sehemu ya baraka kwa mtu fulani. kujitolea kufanya kitu, au kumwachia mtu kiti kwenye daladala. Sehemu ngumu? lakini nzuri. 9.Kaa na watu wenye furaha. Angalia watu unaoshinda nao, unaofanya nao kazi, ni watu wa aina gani. kwa sababu kuna msemo unasema kuwa ukikaa na ua rose utanukia hata kama ulikuwa hunukii. Fanya hivyo na utaweza kufungua mlango mpya kwa ajili yako maishani. utaiona furaha ikitiririka kama mto. 10.Don’t gossip. Kuseng’enya, umbeya, itakusababishia maradhi ya misongo na kukosa furaha. mtu mmbeya hawezi kusaidia kitu. wakati mwingine jitenge na watu kama hawa, au unapoona kuna kutoelewana na wafanya kazi wenzako, jaribu kutulia kwanza , badilisha negative to positive. Sema kitu kizuri kuhusu mtu. ni vizuri. kwa sababu utajiwekea alama nzuri kwako. 11.Tumia muda wako na watu unaowapenda Unapoongea na familia au marafiki kwenye simu , inatia moyo. mawasiliano hayo yanakupa afya na furaha.Fikiri ilivyo vizuri kama utaenda kula na rafiki yako mahali fulani, au kuamua kupika nyumbani , au kucheza na watoto wako kitu kama game, mpira, inafurahisha. 12.Journal Kuandika vitu vya kufanya kwa siku, au kuandika vitu unavyotaka kuvipata, Lengo hili dogo litaongeza IQ yako na kuleta utulivu wa kuboresha ujasiri wako, ukiwa na tabia hii kila siku , furaha haitakosekana kwako na utapata faida ya akili na hisia zako zitakuwa bora. 13.Jizoeze kujijali. Unapojijali ,Utaona faida zake, pamoja na kuondoa stress na wasiwasi, utakuwa mtu wa kuwaza mazuri na utaboresha immunity.pata muda kila siku kufanya kitu kwa ajili ya furaha, kama vile mazoezi, kupika chakula kizuri, kusoma . utaanza kushangaa jinsi ilivyo rahisi kuwa na furaha unapojijali na utaboresha akili yako na mwili wako, na roho yako. Kama unavyojua , kuna njia nyingi zinazotushambulia kwa siku, Ondoka mahali ambapo panaharibu ratiba yako. sasa, kama kitu kingine chochote,mafanikio ni kufanyia kazi. kwa hio pick one, and let the fun begin! ... Read More
Tatizo la Ugumba kwa wanawake  Ugumba ni hali ya mwanamke kushindwa kushika ujauzito. Linaweza kuwa tatizo pia kwa mwanaume lakini katika makala hii tutaona nini kinasababisha tatizo hili kwa upande wa wanawake. Nini husababisha ugumba kwa wanawake? Mayai kutokomaa ipasavyo: Tatizo la mayai kutokukomaa vema ndilo chanzo na sababu kuu ya wanawake wengi kushindwa kushika ujauzito na hii inachukua karibu asilimia 30 ya wanawake wote wagumba. Habari njema ni kuwa tatizo hili linaweza kurekebishwa kirahisi ikiwa mwili utapewa vile viinilishe mhimu vinavyokosekana hadi kupelekea mayai kutokomaa vizuri. Vinavyosababisha mayai ya mwanamke kutokomaa vema: (1) Matatizo ya kihomoni Matatizo katika homoni ndicho chanzo kikuu cha mayai kutunga bila kukomaa vizuri. Hatua za ukomaaji wa mayai zinategemea uwiano mzuri wa homoni na namna zinavyotegemeana katika kufanya kazi. Jambo lolote linalovuruga homoni kubaki katika uwiano wake sawa na wa kutegemeana na wenye kufanya kazi ipasavyo linaweza kupelekea utungaji wa mayai ambayo hayajakomaa vizuri. Kuna sababu kuu mbili zinazosababisha matatizo katika homoni: Ufanyaji kazi usioridhisha wa hypothalamus Hypothalamus ni sehemu ya mbele ya ubongo ambayo ina jukumu la kutuma ishara (signals) kwenda katika tezi ya pituitari ambayo yenyewe tena hutuma uchochezi wa kihomoni kwenda kwenye ovari katika mfumo wa F.S.H na L.H ili kuanzisha ukomaaji wa mayai. Ikiwa hypothalamus inashindwa kufanya kazi zake vizuri kutungwa kwa mayai ambayo hayajakomaa ndiyo kutakuwa ni matokeo yake. Tatizo hili linachukuwa asilimia 20 katika kesi za mayai kushindwa kukomaa kiasi kinachohitajika. Ufanyaji kazi usioridhisha wa tezi ya pituitari Kazi kubwa ya tezi ya pituitari ni kuzarisha na kutoa homoni mbili maalumu kwa ajili ya mfumo wa uzarishaji kufanya kazi zake vizuri ambazo zinajulikana kitaalamu kama ‘Follicle-stimulating hormone (F.S.H)’ na ‘Luteinizing hormone (L.H)’. Mayai yatashindwa kukomaa vizuri ikiwa ama L.H au F.S.H zinatengenezwa chache sana au nyingi sana kuliko inavyohitajika. Hili linaweza kutokea kama sababu ya ajari, uvimbe au kama usawa usio sawa wa kikemikali katika pituitari. (2) Kovu katika Ovari Uharibifu au ajari katika ovari unaweza kupelekea kuzalishwa kwa mayai ambayo hayajakomaa. Kwa mfano, upasuaji mkubwa, uvamizi au upasuaji wa mara nyingi wa uvimbe katika ovari unaweza kusababisha kapsuli ya ovari kupata majeraha au makovu na hivyo kwa namna moja ama nyingine kuweza kuzuia utungwaji wa mayai ambayo hayajakomaa vema. Pia maambukizi katika njia ya uzazi yanaweza kupelekea tatizo hili. (3) Dalili za mwanzo za kukaribia kufunga kuzaa (Menopause) Hii huchangia kwa asilimia chache na kwa sasa halielezeki kisawasawa. Kwamba wanawake wengi wanapokaribia umri wa kuacha kuzaa kuanzia miaka 40 kwenda juu baadhi yao hutokewa na tatizo la kutunga mayai ambayo hayajakomaa vema. Baadhi ya wanawake wanaacha kupata siku zao mapema kabla ya umri uliozoeleka yaani miaka 40 kwenda juu. Kwa sababu hiyo inadhaniwa kwamba uwezo wao wa asili katika kuzalisha mayai unakuwa umepunguwa na wengi wao huwa ni wale walikuwa wakijihusisha zaidi na michezo ya kukimbia au wale wenye historia ya muda mrefu ya kuwa na uzito pungufu na wafanyaji sana wa mazoezi. Tatizo hili pia linaweza kuwa ni la kurithi. (4) Matatizo kwenye kijishimo yai (follicle) katika ovari: Ingawa kwa sasa bado hili nalo halielezeki, hiki kijishimo yai kwa kitaalamu kinajulikana kama ‘’follicle’’ ndicho hupasuka na yai kutoka. Kuna baadhi ya kina mama wanapata dalili za kijishimo yai kutokupasuka “unruptured follicle syndrome” na matokeo yake kila mwezi mama anazalisha yai kama kawaida lakini hiki kijishimo yai kinashindwa kupasuka. Hivyo yai linabaki ndani ya ovari na utungaji wa mimba unashindwa kufanyika. Kinachosababisha ufanyaji kazi dhaifu wa mirija ya uzazi (Fallopian Tubes): Magonjwa katika mirija ya uzazi yanahusika na ugumba kwa karibu ya asilimia 25 ya wanawake wote wagumba. Hali yenyewe inatofautiana toka kwa mmoja hadi kwa mwingine kutoka kugandana au kunatana kidogo hadi kuzibika kabisa kwa mirija. Matibabu ya mirija iliyozibika huhusisha upasuaji au usafishaji wa mwili kwa kula vyakula na vinywaji maalum kwa muda wa majuma kadhaa. Sababu kubwa zinazopelekea kuzibika au kunatana kwa mirija ya uzazi ni pamoja na zifuatazo: (A) Maaambukizi Maambukizi katika njia ya uzazi ambayo yamesababishwa ama na bakteria au virusi na ambayo kwa kawaida ni magonjwa ya kuambukizana kwa njia ya tendo la ndoa, maambukizi haya kwa kawaida husababisha muwasho au kuungua na kupelekea makovu na uharibifu. Magonjwa ya zinaa kama vile kisonono na mengineyo yanaweza kuwa chanzo cha ugumba kwa wanawake wengi hasa ikiwa hayatatibiwa mapema. (B) Magonjwa yasiyo ya kawaida Magonjwa yasiyo ya kawaida ni pamoja na ugonjwa wa kidole tumbo (appendicitis) na uvimbe katika utumbo mpana (colitis), magonjwa ambayo husababisha muwasho au kuungua chini ya uvungu wa utumbo mkubwa na kuiathiri mirija ya falopiani na kama matokeo yake makovu na kuzibika kwa mirija ya uzazi hutokea. (C) Upasuaji uliopita Upasuaji una chukua nafasi kubwa katika kusababisha ugumba kutokana na matokeo yake ya kusababisha magonjwa ya mirija ya uzazi na uharibifu utokanao na huo upasuaji. Upasuaji katika utumbo mkubwa unaweza kupelekea kunatana au kugandana kwa mirija ya uzazi kutakakopelekea mayai kushindwa kusafiri kirahisi katika mirija hiyo ya uzazi. (D) Mimba kutungwa nje ya mji wa uzazi: Hii ni wakati mimba inapotungwa katikati ya mirija ya uzazi yenyewe. Katika hali kama hii hata kama kutatokea bahati kiasi gani bado kunaweza kusababisha uharibifu katika mirija na hali hii ni moja ya hali mbaya sana kiafya na kimaisha. (E) Hali ya kurithi Kwa nadra au kwa asilimia fulani ndogo baadhi ya wanawake huzaliwa na hali ya kuwa na mirija isiyo ya kawaida kwa uzazi na kwa kawaida hali hii huambatana na mji wa uzazi usio wa kawaida pia. . (5) Sababu za kitabia: Inajulikana wazi kwamba baadhi ya tabia na namna tunavyoishi kunaweza kupelekea wanandoa wakashindwa kupata mtoto. Kwa bahati nzuri nyingi kama si zote ya hizo tabia zinaweza kurekebishika au kuachwa kabisa na kupelekea siyo tu kuwa na uwezo wa kuzaa bali pia kuwa na afya nzuri kwa ujumla. Sababu hizo za kitabia ni pamoja na zifuatazo: Lishe na mazoezi Ili mfumo wa uzazi uwe na uwezo mzuri unahitaji vitu viwili mhimu, lishe kamili na mazoezi. Wanawake wenye uzito uliozidi sana au wenye uzito pungufu sana wanaweza wakapatwa na tatizo la kutopata ujauzito kirahisi. Uvutaji sigara Uvutaji wa sigara una mchango mkubwa na ugumba. Uvutaji sigara husababisha uzarishwaji wa mbegu chache kwa mwanaume (lower sperm count) kwamba mwanaume anatoa mbegu chache sana ama pungufu wakati huo huo uvutaji sigara huchangia katika tatizo la kutoka kwa mimba, kuzaa kabla ya miezi 9 (njiti), na kuzaa mtoto mwenye uzito mdogo kwa wanawake. Unywaji pombe Unywaji pombe kupita kiasi una mchango mkubwa sana katika ugumba na hii hata ikitokea mama akapata ujauzito kama bado anaendelea kunywa pombe inaweza kupelekea matatizo hata kwa mtoto mtarajiwa. Unywaji pombe pia huchangia uzarishwaji wa mbegu chache kwa wanaume. Madawa ya kulevya Utumiaji a madawa ya kulevya kama bangi na mengine ya kujidunga kwa sindano kunaweza kuwa sababu ya kuzalisha mbegu chache kwa wanaume. Utumiaji wa dawa za kulevya kama ‘Cocaine’ kwa mama mjamzito kunaweza kusababisha mtindio wa ubongo na matatizo katika figo kwa mtoto mtarajiwa. Matumizi ya madawa ya kulevya inafaa yaepukwe wakati wa kutafuta ujauzito na wakati wa ujauzito. Utowaji mimba Utowaji mimba wa mara kwa mara pia unahusika sana na tatizo la ugumba kwa karibu ya asilimia 20. Utowaji mimba unaweza kusababisha makovu katika mji wa uzazi na hata kuharibika kabisa kwa mji wa uzazi ikiwa utowaji huo haukufanyika kitaalamu au unafanyika mara kwa mara. (6) Sababu za ugumba za kimazingira: Uwezo wa kushika ujauzito unaweza pia kuathiriwa kutokana na kuwa karibu na baadhi ya kemikali au sumu katika maeneo ya kazi au makazi. Vitu viwezavyo kusababisha mabadiliko, dosari za kuzaliwa, utokaji mimba, au utasa huitwa ‘Sumu kwa mfumo wa uzazi’. Kamikali zifuatazo zinahusishwa na ugumba au utasa: Risasi (Lead) Kuwa karibu na kemikali au sumu zinazounda risasi kunaweza kuwa sababu ya ugumba. Risasi hupelekea kuzalishwa kwa mbegu zisizo za kawaida kwa wanaume zijulikanazo kwa kitaalamu kama ‘teratospermias’ na inafikirika pia kuhusika na utokaji mimba kusiko kwa asili (artificial abortion). Baadhi ya matibabu na madawa ya hospitalini Kuwekwa kwenye matibabu yanayohusisha mionzi (x-rays), mionzi ya kawaida au hata ile ya kutibia kansa (chemotherapy), kunaweza kusababisha matatizo katika uzarishwaji wa mbegu kwa mwanaume na wakati huo huo kuchangia kwa sababu kadhaa zinazopelekea kutungwa kwa mayai ambayo hayajakomaa vizuri. Pia matumizi ya dawa za kuzuia ujauzito kwa muda mrefu yamekuwa yakihusishwa na ugumba kwa miaka ya hivi karibuni ingawa bado kuna mjadala mkubwa katika hili. Ethylene Oxide Hii ni kemikali inayotumika kusafishia vifaa vya upasuaji, pia hutumika katika kutengeneza baadhi ya sumu za kuua wadudu. Ethylene oxide inaweza kupelekea matatizo katika uzazi hasa katika miezi ya mwanzo mwanzo ya ujauzito na inahusishwa sana na tatizo la utokaji mimba katika miezi ya mwanzo ya ujauzito (early miscarriage). Dibromochloropropane (DBCP) Hii pia ni kemikali au dawa inayotumika katika kuua wadudu, ikiwa unafanya nayo kazi kila mara inaweza kusababisha kutungwa kwa mayai yasiyokomaa vizuri, kuelekea mapema kwa ukomo wa kutokuzaa kabla hata ya miaka 40 au 45 (early menopause) na kadharika. (7) Sababu zingine zinazoweza kusababisha ugumba kwa mwanamke: Karibu asilimia 10 ya ugumba kwa wanawake ni matokeo ya mji wa uzazi usio wa kawaida (abnormal uterus). Hali zingine ni pamoja na uvimbe katika kizazi, kugandana au kunatana kwa mji wa uzazi na mirija ya uzazi. Karibu asilimia 3 ya ugumba kwa wanawake ni matokeo ya matatizo ya ute usio wa kawaida katika mlango wa kizazi (femaleís cervical mucus). Ute ute huu unahitaji kuwa na hali fulani maalumu kwa mbegu za kiume kuweza kuogelea kirahisi katikati yake. Chanzo kikubwa cha tatizo hili ni usawa usio sawa wa homoni za kike ambapo homoni ya uzazi ya kike iitwayo ‘estrogen’ yaweza kuwa ni chache sana au homoni nyingine iitwayo ‘progesterone’ yaweza kuwa ni nyingi sana tofauti na inavyohitajika. Vitu vya kuepuka kwa mtu mwenye tatizo la ugumba: ChipsiVinywaji baridiKaffeinaNyama nyekunduVilevi ... Read More
SABABU YA KWELI WANAWAKE KUENDELEA KUTEMBEA NA WANAUME WALIO OA  Jane ni mwanamke mwenye mafanikio, anamiliki kampuni ya kutengeneza mifuko ya plastic, ana studio. Ana akili , anavutia na ni mwenye ujasiri. Pia anatembea na mume wa mtu. Amekuwa akiwauliza rafiki , familia yake ambao wanafahamu kuwa kitu gani kinamfanya mwanamke mwenye mafanikio, akili na ujasiri kutembea na mume wa mtu kwa miaka zaidi ya mitatu? Hamu ndio Inayoanza Mwanaume ambaye ameoa anapomkaribia mwanamke , anakuwa na hatari— hatari ambayo inaonyesha kumuhitaji zaidi. Kuwa na muda naye. Huenda kwa meseji au kupata chakula pamoja kwa siri, au kulala nae kwa siri. Huonyesha kuwa na majukumu kama mwanaume single. Lakini mwanaume single huandaa date. Huwa na sababu nyingi za kufanya hivyo, na ukiri wao huwa ni wa makini na huonyesha kuwa hawako interested. Hujikuta wameingia kwenye majukumu ambayo hakuwa amejiandaa. Kwa ushindani, kazi ya mwanaume aliyeoa Inamlinda kutokana na nia yake kwa mwanamke single ili kuonyesha hamu yake. Kama hataweza kuonyesha hisia zake kwa kumtazama macho yake, sauti yake, kumsugua mwanamke mgongo wake, kumfanyia massage kwenye mabega, mwanamke atajuaje kama anamtaka? Na ataendeleaje kubaki nae kama hamtimizii haja zake? Kwa kufanya hayo anaweza kumuwekea ulinzi, mahusiano yao kukomaa na kuwa mazuri na kuwa ya kawaida. Lakini akili Itakuja. Marafiki aliowaambia watamkumbusha.Ni mume wa mtu. Familia watamuuliza , bado yuko na mke wake? Wakati anapoanza kujiuliza ndani yake , mume alienae, Ataanza kuwa na njia mbili. Kwa wanawake wengi, hio imepitwa na wakati. Kwa wengine mchezo utaendelea—kwa kufahamu maamuzi haya…tuangalie sasa 1.Wakati mwanaume anapotoka nje, uwezekano mkubwa hana furaha ndani ya nyumba yake. 2Talaka zinaongezeka . ndoa zinafikia mwisho, na wanaume wanaoa tena. 3.Uzinzi unaongezeka kwa wanaume. Huenda kuishi muda mrefu peke yao sio mpango mzuri. Kwa mtu kama Jane kuishi maisha kama hayo, huenda ni katika kumpata mtu sahihi na kumuondoa kwa mke wake hata kama kutakuwepo hatari katika hisia zake. Mwanamke kama Jane ni wepesi wa kujifunza zaidi kuhusu tabia za wanaume ambao wanacheat kabla ya kuamua kuingia kwenye mahusiano ya kudumu. Wengi wa wanaume wanasema , sababu kubwa ya kucheat ni kukosa sex Ni kiasi kidogo sana cha wanaume ambao hupotea katika mapenzi ya nje Baadhi ya wanaume wanaocheat walitoa taarifa kuwa wanafanya hivyo kwa wenza wengi karibu miaka yote Kwa kulinganisha wanawake na wanaume. Wanawake wao huingia kwenye mahusiano kwa mwanaume aliyeoa kwa sababu ya kuwapenda. Lakini sio nzuri kama mtu ameoa ni bora kujiheshimu na kumuheshimu mke wake , Na kama kuna tatizo ni vizuri kurekebisha kuliko kwenda kutafuta majibu ya tatizo lako nje.Kwa nini nasema hivi , ni kwa sababu ipo siku mwanamke huyo atahitaji kuwekwa wazi , utafanyaje na wewe ulikuwa ni mwizi. kwa upande wa mwanamke Utavunjika moyo, inapofika wakati kama huo.Maumivu ya kuachwa na mwanaume aliyeoa ni makubwa kuliko ya kuachwa na mwenza ambaye ni wako kabisa. Black woman hugging her knees 1.Utajisikia kama mkosaji mara mbili. Kwamba hukuweza kumpata mtu ambaye tayari kwanza alikuwa ameoa na amekuacha baada ya kuridhika kwake. 2.Wasaliti wanaokatiza mahusiano huwa wanaonyesha kabisa kuwa hawana hisiana za kutosha kwako. Wanakuchukulia kama wewe ni msichana mkubwa, na unaelewa kitu gani unachokifanya. 4.Mfumo unaompa support unaweza ukawa upo gizani. HUenda ni aibu au hamu ya kumlinda msaliti au vyote. Hakuna mtu ambaye anafahamu. Kama wapo basi ni wa katibu sana. Kwa hio watu kama Jane wataepuka vipi hatari inayotokana na aina hii ya mahusiano? Ukweli ni kwamba, ufahamu una nguvu.Kama msomaji unahusika na mume wa mtu, rudia tena kusoma makala hii kwa makini kabla hujaendelea zaidi. Maisha ni mafupi.Muda wa kumsaidia mume wa mtu ambaye amekosa kitu fulani kwa mwenza wake umekwisha. Mwache akatengeneze kwa mwenza wake. Wanaume Single wako wengi wanakusubiri na hawana hatari kama hizo. Hata kama atakuonyesha kuwa wako cool mwanzoni usidanganyike. ... Read More
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments: